Iringa: Ajali yaua Mume na Mke

Watu watatu amabao walikuwa wakisafiri kuelekea mkoani Ruvuma kwenye msiba akiwemo mume na mke pamoja na mfanyakazi wa ndani wamefariki dunia papo hapo ktk ajali ya barabarani baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori lenye namba za usajili T 866 DMC aina ya MITSUBISH CANTER.

Imeelezwa kuwa watu hao walikuwa wakisafiri kwa kutumia gari aina ya TOYOTA RAV4 lenye namba za usajili T 795 DGD na kupata ajali ktk eneo la Kisolanza wilayani Iringa ktk barabara kuu ya Dar-Ruvuma.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Bw Julius Mjengi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.