F Ushindi wa Anthony Joshua dhidi ya Takam wapingwa na mashabiki | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Ushindi wa Anthony Joshua dhidi ya Takam wapingwa na mashabiki

Hata kabla ya mpambano bondia Anthony Joshua alishatabiri kwamba inaweza kumchukua raundi 10 kumpiga mpinzani wake Carlos Takam na hakufanya kosa na alitimiza ahadi yake.

Pamoja na kuzomewa na mashabiki wengi waliokuwepo uwanjani hapo kushuhudia pambano hilo lakini Anthony Joshua amefanikiwa kutetea ubingwa wake wa IBF.

Muamuzi wa mpambano huo aliamua kuukatisha katika raundi ya 10 baada ya mpinzani huyo wa Anthony Joshua kuonekana anavuja damu nyingi kwenye uso wake juu ya jicho kutokana na ngumi za AJ.

Lakini watu walizomea maamuzi hayo kwani pamoja na kuvuja damu lakini Takam alionekana bado yuko fiti na ana nguvu kwani alikuwa akiendelea kurusha ngumi japokuwa alikuwa amepasuka usoni.

Wengi baada ya mchezo huo wanaamini Takam alionewa na muamuzi kwa kukatisha pambano hilo na badala yake angeendelea kumpa muda wa kusimama ulingoni kupigana.

Baada ya mpambano huo promota wa Joshua bwana Eddie Hean amewaahidi mashabiki wa Joshua kwamba mwakani Joshua atakuwa na mpambano mkubwa mwingine huku Tyson Furry akipewa nafasi.

Anthony Joshua amejitamba kwamba angeweza kummaliza na kumuumiza zaidi Carlos Takam lakini maamuzi ya muamuzi wa mpambano huo yamemuokoa Mcameroon huyo na sasa Aj anakuwa ameshinda mapambano 20 mfululizo.