F Pogba kurudi dimbani na muonekano mpya | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Pogba kurudi dimbani na muonekano mpya

Mshambuliaji  wa Manchester United, Paul Pogba anayetumiakia adhabu ya kukosa mechi tatu, amegeukia mitindo ya nywele ambapo ameonekana akiwa amekoleza rangi kwenye kiduku chake.

Mchezaji huyo aliikosa mechi ya watani ya Manchester United na Manchester City Jumapili iliyopita na hakuwepo kabisa uwanjani. Pia ameikosa mechi ya United na Bournemouth.

Jana Alhamisi, mchezaji huyo mwenye mika 24 alituma picha yake akionyesha mtindo mpya wa nywele kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo, mchezaji huyo amekuwa akijifua mazoezi binafsi ili kuhakikissha anajiweka fiti na mechi zinazofuata.