Baada ya kufuta picha za Diamond Platnumz, Rick Ross afunguka


Rapa maarufu duniani Rick Ross wiki hii amefuta karibia picha zote za msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambazo awali alikuwa ameziposti kwenye ukurasa wake wa Instagram kitu ambacho kilizua gumzo kwa mashabiki wake nchini Tanzania.

Kama ulikuwa unaamini kuna bifu kati ya wawili hao, ukweli ni kwamba wawili hao bado wapo kwenye mahusiano mazuri ila ni ishu tu za kibiashara ndio zimewatenganisha kwa sasa ndio maana alifuta picha hizo.

Kwani Rick Ross jana alitumia muda wake kutoa maoni kwenye posti ya Tarehe 01 Desemba 2017 ambapo aliweka promo ya wimbo mpya wa Diamond kipindi hicho akiwa amewashirikisha kundi la Morgan Heritage ‘Hallelujah’ na kuandika kuwa “Diamond iz a Legend“.


Hata hivyo, kuthibitisha hilo kuwa Rick Ross na Diamond wapo poa ila ni ishu tu za kibiashara ndio zimepelekea Rick Ross kufuta picha hizo, Moja ya mameneja wa Diamond, Sallam amethibitisha hilo kwa kuandika “Nafahamu mastaa wengi wakiposti vitu vya support au tangazo ikifika muda wanafuta hata Diamond mwenyewe anafuta zikishapita muda wake“