Hizi ndizo timu 5 ambazo zinaning'inia Ligi Kuu

Timu tano za Ligi Kuu zimejikuta kwenye mstari ambao sio wa mafanikio wala hasara kwao.

Hizi ni timu ambazo zinaning'inia kwenye msimamo wa ligi katika nafasi ambazo sio zile za kushuka daraja, kuchukua ubingwa wala kumaliza katika nafasi nne za juu msimu huu.

Kundi hili linajumuisha timu za Lipuli, Ndanda, Mbao, Mwadui na Mbeya City ingawa nazo kama zikishindwa kuchanga vyema karata mzunguko wa pili, zinaweza kujikuta zimeangukia kwenye kundi la timu zinapambana kutoshuka.