Kenya kuweka rekodi kombe la Dunia

Aden Marwa ni miongoni mwa waamuzi wasaidizi 10 kutoka Afrika watakaosimamia mechi za kombe la dunia.

Mwamuzi huyo mwenye uzoefu wa miaka 7 akifanya kazi na shirika la FIFA,alifanikiwa kuorodheshwa kwenye orodha ya mwisho kwa ajili ya kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil. Hata hivyo hakufanikiwa kusimamia mechi yeyote.

FIFA imechagua maafisa 6 kutoka barani Afrika kusimamia mechi za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Urusi.

Pamoja na hao waamuzi wasaidizi 10 wametoka barani Afrika, kwa ujumla maafisa 99 wamechaguliawa kusimamia michuano hiyo.

Aden Marwa ana uzoefu wa kuwa mwamuzi msaidizi katika michuano ya kombe la dunia la vilabu 2016 nchini Japan.

Alitajwa kuwa mwamuzi msaidizi wa CAF katika shirikisho la kombe la FIFA 2017 na alishiriki pia mwaka 2012,2013, na 2015 kwenye kombe la mataifa ya Afrika pamoja , kombe la dunia la walio chini ya miaka 17 , michuano ya CAF ya chini ya miaka 23 na kombe la dunia la vilabu la FIFA