Utafiti unaonyesha jinsi ‘Smartphone’ zinavyoua kumbukumbu za binadamu

Utafiti mpya kutoka nchini Uingereza unaonesha kwamba ongezeko la simu aina ya smartphone na mitandao ya kijamii linalosababisha tabia wa watu kupiga picha mara kwa mara linasababisha watu kupoteza kumbukumbu.

Utafiti huo unaeleza kuwa kupiga picha muda wote kunasbabisha watu kupoteza kumbukumbu ya vitu ambavyo wanaviona na hii ni athari kubwa kwa ustawi wa mtu.

Wanasayansi hao ambao wamechapisha utafiti huo kwenye jarida la Journal of Experimental Social Psychology wameeleza kuwa ongezeko la mitandao ya kijamii halijawa tu athari kwa afya za watumiaji bali hata maisha yao ya kawaida.