Hatimaye Mbunge wa Tarime Vijijini(CHADEMA), John Heche leo amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kuunganishwa kwenye kesi namba 112/2018 inayowakabili Viongozi wengine wa Chama hicho.
Wakili wa serikali, Faraja Nchimbi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa wanaomba kumuunganisha Heche katika kesi inayowakabili wenzake ambapo yeye atakuwa mshtakiwa wa 8 ambapo amepewa kwa masharti ya dhamana kama watuhumiwa wengine.
John Heche ameachiwa kwa masharti ya dhamana na anahitajika kuwasili cha Polisi Central kila Ijumaa huku kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 16 Aprili mwaka huu.