Baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole kumtuhumu Mhe. Zitto Kabwe kupotosha taarifa za CAG kuhusu kupotea kwa shilingi trilioni 1.5, kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo ameibuka na kujibu mapigo.
Zitto ametumia mtandao wa Twitter kujibu tuhuma hizo za Polepole kwa kumwambia amekuwa Mwenyekiti wa PAC/POC kwa miaka nane hivyo anafahamu kile anachokisema.
“Serikali ya CCM ilidhani Watanzania ni mandondocha,wanapelekwa pelekwa tu. Nimekuwa Mwenyekiti wa PAC/POAC kwa miaka 8. Ninajua ninachosema.” ameandika Zitto.
“Jumla ya TZS trilioni 1.5 hazina maelezo ya matumizi yake Katika mwaka 2016/17. Sitajibishana na Mwenezi wa CCM, yeye size yake @AdoShaibu,” ameongeza.