Emmanuel Mbasha afunguka kuwa kwenye kundi la East Zu pamoja na marehemu Ngwea

Fahamu kuwa Mwimbaji wa nyimbo za Gospel Emmanuel Mbasha aliwahi kuwa kwenye kundi la East Zu pamoja na Marehemu Albert Ngwea, Dark Masta huko jijini Dodoma kabla ya kuanza kuimba nyimbo za Gospel.

Emmanuel Mbasha ameyaongea hayo kupitia kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM na kusema kuwa aliacha kufanya muziki wa Bongo Fleva baada ya kuokoka na kusema kuwa watu wengi hudhani kijana akimrudia Mungu basi anakuwa na matatizo makubwa au majaribu.

“Niliacha kufanya Bongo Fleva baada ya kuokoka na kumpokea Bwana yes wengi wanadhani kijana akimrudia Mingu basi anakuwa na matatizo makubwa lakini kwa upande wangu mimi niliokoka tu sikuwa na tatizo lolote wala majaribu”

“Wakati nipo mkoa tulikuwa tunafanya nao muziki baadaye niliamua kufanya muziki wa Gospel lakini nimekuwa nikishauri wasanii wenzangu waje huku nilipo tumwimbie Mungu”>>> Emmanuel Mbasha