F Matonya amchambua Fid Q | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Matonya amchambua Fid Q


Msanii wa Muziki, Matonya amefunguka kumshirikisha msanii wa Hip Hop, Fid Q kwenye wimbo wake mpya wa 'Nisulubishe'.

Matonya amesema kuwa ukizungumzia wana Hip Hop bora msanii huyo hawezi kukosa kwasababu ana radha ya tofauti na watu wengine.

"Ukizungumzia wana Hip Hop bora kabisa Fid q hawezi kukosa, nimempa Fid Q nafasi ndogo kwasababu watu wamezoea kwamba mtu akishirikishwa vrese moja nzima ndefu na vitu kama hivyo," amesema Matonya kwenye e News ya EATV.

"Kwenye utengenezaji wa muziki tunahitaji kupata test , tunahitaji kupata muziki mzuri, kwahiyo mziki mzuri unatengenezwa kwa njia nyingi,  kumuweka pale mwanzo watu wamezoea kumuweka verse ya pili, Fid Q ana radha yake toauti na watu wengine kwahiyo nikaona akifungua alafu nikishikilia pale tunaweza tukapata combination moja kali na ndicho ambacho kimetokea hatukutaka kufanya kitu ambacho watu wamekizoea sana."   

Wasanii hawa wameshawahi fanya nyimbo mbili wa kwanza ' usinikubali haraka' na mwingine 'Tax Bubu'.