Muziki wa Bongo Fleva ni kiwanda chenye wafanyakazi (wasanii) zaidi, wapo walioanza na kiwanda hiki mwanzo, wengine walijiunga katikati ya safari na kuna wapya wanajiunga sasa. Wote hawa kazi yao ni moja tu, si nyingine bali kutoa burudani kwa mashabiki wao ambao ndio wanunuzi wa bidhaa husika.
Kwa
mwaka 2018 kila mmoja amefanya kazi kwa kiwango chake kutokana na malengo
aliyojiwekea na wengine kadiri mazingira yalivyoruhusu. Vyovyote ilivyokuwa,
napenda kuangazia wasanii 10 kutoka kwenye muziki hao ambao wamefanya vizuri
zaidi kwa mwaka huu.
1.
Harmonize
Mwaka
2018 umekuwa wenye mafanikio makubwa sana kwa Harmonize kimuziki
ukilinganisha na miaka mingine. ametoa nyimbo ambazo zimefanya vizuri zaidi na
pia ameweza kushirikiana na wasanii wakubwa kutoka Tanzania na mataifa mengine
ya Afrika.
Muimbaji
huyo ambaye ndiye msanii wa kwanza kusaini kwenye lebo ya Diamond Platnumz
'WCB' mwaka huu ameweza kufanya kolabo na wakongwe wa Bongo Fleva kama Dully
Skyes na Professor Jay ambao wote wawili walishawahi kufanya kazi na Diamond
'Chibu Dangote' na kufanya vizuri.
Pia
ameweza kufanya kazi na wasanii wakali kutoka Afrika kama Eddy Kenzo (Uganda),
Marina (Rwanda), Willy Paul (Kenya), Sarkodie (Ghana). Wengine ni Emma Nyra,
Skales, IYO na OmoAkin, wote kutokea Nigeria.
Wimbo
wake unaokwenda kwa jina la Kwangwaru aliomshirikisha Diamond unatajwa kama
wimbo wenye mafanikio makubwa zaidi kwenye Bongo Fleva kwa mwaka huu, kivipi?.
Ndio
wimbo pekee ulitazamwa zaidi kwenye mtandao wa YouTube kwa mwaka huu, hadi sasa
una views Milioni 38. Video ya wimbo huu ilitoka April 14, 2018 iliweza
kuweka rekodi ya kufikisha views Milioni 10 kwa kipindi cha mwezi mmoja
kitu ambacho hakuna msanii wa Tanzania aliyewahi kufanya hivyo.
Hapo
awali wimbo wa Harmonize ulikuwa ukiongoza kutazamwa zaidi YouTube ni Bado
ambao pia alimshirikisha Diamond. Wimbo huu ulitoka miaka miwili iliyopita na
hadi sasa una views Milioni 20 na uliwekwa kwenye mtandao huo February 29,
2016.
Ukiachana
na hilo pia Harmonie kwa mwaka amefanya ziara ya kimuiki (music tour) nchini
Marekani kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja ambapo alifanya show zake
Houston TX, Dallas TX, Oakland CA, Seattle WA, Atlanta GA, Los Angeles CA,
Private Event na Washington DC.
2.
Diamond Platnumz
Ni
miaka mingi sasa amekuwa akifanya vizuri, kila mwaka amekuwa na nyimbo ambao
zinafanya vizuri kwenye chati za muziki, tuzo, mtaani na mtandaoni (streaming),
achana na hilo.
Kwa
mwaka huu amesumbua na albamu yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu 'A
Boy From Tandale' ikiwa ni albamu yake ya pili tangu alipotoka kimuziki mwaka
2009.
Albamu
ya A Boy From Tandale ilizinduliwa rasmi March 14, 2018 Nairobi nchini
Kenya ambapo wasanii wote kutoka WCB walishiriki pamoja na msanii kutokea
Marekani, Omario ambaye pia ameshiriki kwenye wimbo wake unaokwenda kwa jina la
African Beauty.
Wasanii
kutoka nje ya Tanzania walioshiriki kwenye albamu hiyo yenye nyimbo 18 ni kundi
la Morgan Heritage (Jamaica), Jah Prayzah (Zimbabwe), Omario, Rick Ross na
Ne-Yo (wote Marekani), pia kuna Tiwa Savage, Davido, P Square na Mr. Flavour
hawa wote kutokea Nigeria.
Licha
ya albamu hiyo kutofanyiwa uzinduzi nchini Tanzania, Diamond alifanya ziara
(tour) kwa ajili ya kuitangaza nchini Marekani kwa kipindi cha mwezi mmoja,
wapenda muziki wa Afrika kutoka maeneo ya Texas, Los Angeles na Chicago
walimpata mubashara kabisa Chibu Dangote.
3.
Vanessa Mdee
Umekuwa
ni mwaka mwingine wenye mafanikio kwa muimbaji huyo wa kike wenye uwezo wa
kuimba kwa ufasaha lugha zaidi ya tatu (Kiswahili, Kingereza, Kifaransa na
Kihindi). Ni Vee Money au Cash Madam, licha ya kutoa nyimbo kadhaa ningependa
kuangaza mafanikio yake katika mambo manne;
Mosi;
Lebo, ukiachana na Diamond Platnumz na Alikiba, Vanessa Mdee pia ana lebo yake
ya muziki inayofahamika kama Mdee Music ikiwa na wasanii watatu, Vanessa
mwenyewe, Brian Simba na Mimi Mars.
Akiwa
kama msimamizi mkuu wa lebo hiyo, Vanessa ameweza kumsimamia Mimi Mars na
kutoa EP yenye nyimbo sita na kuwa msanii pekee wa kike Tanzania kufanya
hivyo kwa mwaka huu. Pia Mimi Mars anatarajiwa kuonekanekana kwenye msimu mpya
wa Coke Studio Afrika.
Pili;
mwaka huu Vanessa Mdee ametoa albamu yake ya kwanza, Money Mondays tangu
alipoanza muziki. Albamu hiyo yenye nyimbo 17 imefanya vizuri kimauzo kwa pande
zote. Wasanii aliowashirikisha kwenye albamu hiyo ni kama Maua Sama, Joh
Makini, Reekado Banks (Nigeria) Cassper Nyovest na AKA (Afrika Kusini).
Tatu;
Vanessa Mdee ni miongoni mwa wasanii watatu pekee wa Tanzania waliotumbuiza
kwenye tamasha la One African Music kwa mwaka 2018.
Wasanii
wengine kutoka Bongo walioshiri kwenye tamasha hilo lilofanyika November 16,
2018, Dubai, ni Nandy na Diamond.
Tanzania
ndio nchi iliyotoa wasanii wengi Afrika Mashariki, Kenya iliwakilishwa na
msanii mmoja, Akothee. Si mara ya kwanza kwa Vanessa kushiriki tamasha hilo
ambalo limekuwa likikutanisha wasanii kubwa wa Afrika, hivyo muimbaji huyu
anazidi kudumu na ukali wake.
Nne:
ziara ya kimuki (music tour), kwa kushirikiana na Jux ambaye ni mpenzi
wake, mwaka huu wamefanya ziara yao iliyojulikana kama 'In Love &
Money'. Ziara hii iliyopita kwenye mikoa ya Mtwara, Mwanza, Dodoma, Arusha na
Dar es Salaan ilikuwa yenye mafanikio makubwa zaidi kwani kila walipoenda watu
walifurika.
4. Maua
Sama
Hakuna
ubishi kuwa wimbo wa Maua Sama, Iokote umefanya vizuri zaidi kuliko nyimbo za
wasanii wote wa kike zilizotoka ndani ya mwaka huu.
Ni
wimbo wake wa tatu kutoa ndani ya mwaka huu baada ya Nakuelewa na Amen
ambao ameshirikiana na Ben Pol ukiwa pia ni wimbo wao pili kufanya pamoja.
Iokote umekuja kuandika histori nyingine kwenye maisha ya kimuziki kwa upande
wa Maua Sama, kivipi?.
Maua
Sama amekuwa msanii wa kwanza wa kike Tanzania kwa wimbo wake kufikisha views
Milioni 1 kwenye mtandao wa YouTube ndani ya wiki tatu bila video
rasmi.
Wakati
anaweka rekodi hiyo alikuwa akishikiliwa na Jeshi la Polisi, Dar es Salaam kwa
kile kilichoelezwa ni kusambaza video ya watu waliokuwa wakicheza wimbo
huo huku wakichezea fedha kwa kuzikanyaga kitu ambacho ni kinyume cha sheria.
Hata
hivyo baada ya wiki moja alitoka na kutoa video rasmi ya wimbo huo ambayo pia
imefanya vizuri kuliko video zake zote alizotoa tangu alipoanza muziki, hadi
sasa ikiwa na views zaidi Milioni 5.7.
5.
Mbosso
Huyo ni
msanii wa mwisho kusainiwa na lebo ya WCB, usiku wa January 27, 2018 ndipo
alitambulishwa rasmi na kutoa wimbo wake wa kwanza unaokwenda kwa jina la
Watakubali.
Utakumbuka
baada ya kuvunjika kwa kundi la Yamoto Band kila msanii alianza kutoa kazi zake
binafsi (solo project). Mbosso ndiye alikuwa msanii wa mwisho kutoa wimbo baada
ya wenzake kumtangulia, hata hivyo amekuwa mwenye mafanikio makubwa zaidi.
Baada
ya hapo ameweza kufanya vizuri na nyimbo kama Nadekezwa, Hodari, Nipepe na
nyinginezo. Nyimbo hizi tatu nilizotaja, zote zina views zaidi ya Milioni 4.5
kwenye mtandao wa YouTube, si kitu kirahisi kwa muda huo tangu aliposaini WCB.
Pia
imekuwa ni mapema kwake kufanya wimbo na Diamond Platnumz ukilinganisha na
wasanii wengine wanaosaini kwenye lebo hiyo. Wimbo Jibebe waliofanya pamoja na
Lava Lava ni miongoni mwa nyimbo chache kali zilizosumbua kila kona kwa mwaka
huu.
6. Navy
Kenzo
Ukiachilia
mbali mahusiano ya kimapenzi waliyonayo na kama wazazi, hili ni kundi la
waimbaji ambalo limefanya vizuri kwa mwaka huu. Wametoa nyimbo mbili pekee
ambazo ni Fella na Katika na zote zimefanya vizuri.
Nyimbo
hizi zimekuja mara baada ya kujaliwa kupata mtoto mmoja ambaye wamempa jina la
Gold na kuchukua mapumziko mafupi kimuziki kwa ajili ya malezi, ujio wao mpya
umekuwa wenye nguvu kubwa zaidi.
Wimbo
wao uitwao Katika hadi sasa una views zaidi ya Milioni 8.8 kwenye mtandao wa
YouTube tangu ulipotoka September 27, 2018. Pia wimbo huu umeweza kushika
nafasi ya kwanza kwenye chati za muziki za BBC Radio 1Xtra nchini Uingereza.
Utakumbuka
producer Nahreel ambaye ni msanii wa kundi hili, mwaka huu pia ametengeneza
wimbo wa Kombe la Dunia Russia 2018, wimbo huo ni ule alioshiriki Diamond
Platnumz na Jason Derulo kutoka Marekani. Huu ni wimbo wa tatu kwa Nahreel
kufanya na Diamond baada ya Nana na Katika.
7.
Alikiba
Licha
ya kutoa nyimbo kadhaa na kufanya vizuri, kwa mara ya kwanza mwaka huu ameweza
kutambulisha wasanii kutoka kwenye rekodi lebo yake 'Kings Music' ambayo
ilikuwa ikizungumziwa kwa kipindi kirefu.
Kings
Music kwa sasa ina wasanii wanne na Alikiba mwenyewe ambaye pia anafanya kazi
na RockStar Africa akiwa kama Director of Music and Talents.
Utakumbuka
July, 2017 Alikiba alitangazwa kuwa miongoni mwa wamiliki wa kampuni ya
Rockstar4000 Music Entertainment Co & Rockstar Television ambayo kwa sasa
inajulikana kama RockStar Africa.
King
Music ndani ya mwaka huu wameweza kutoa nyimbo mbili ambazo ni Mwambie Sina na
Toto. Alikiba si msanii wa kutoa nyimbo kila mara, kwa mwaka jana aliweza kutoa
wimbo mmoja pekee, Seduce Me lakini kwa mwaka huu ametoa nyimbo mbili ambazo ni
Mvumo wa Radi na Kadogo na zote zimefanya vizuri.
Pia
ameweza kufanya show kubwa ndani na nje ya Tanzania, moja wapo ni tamasha la
Africa All Star Music Fest lilofanyika nchini Canada, August mwaka huu ambapo
Alikiba alitumbuiza jukwaa moja na wasanii kama Yemi Alade, Falz The Bahd
Guy, Sheebah, Dj Spinal, Zahara, Nonso Amadi na Nsoki.
8.
Nandy
Ukiachana
na nyimbo kama Subalkheri Mpenzi na Aibu alizotoa kwa mwaka huu, pia huyu ni
msanii wa pili wa kike Tanzania kutoa albamu kwa mwaka huu.
Ameweza
kutoa albamu yake ya kwanza tangu kuanza muziki, The African Princess ikiwa na
nyimbo 13 na ikiwa imemshirikisha msanii mmoja pekee ambaye ni Aslay. Albamu
hii imeuzwa kwa mfumo wa nakala za kawaida (hard copy) pamoja na mtandaoni
(streaming & downloads).
Pia
ameweza kushinda tuzo mbalimbali kama African Entertainment Awards AEA USA 2018
zilizofanyika October 20, 2018, New Jersey nchini Marekani, Nandy alishinda
kwenye kipengelee cha Best Single Female kupitia wimbo wake uitwao Kivuruge.
Huyu
ndiye msanii pekee wa kike kutoka Tanzania kushinda tuzo hiyo kwa mwaka huu.
Wasanii wengine walioshinda ni Diamond aliyechukua mbili kwenye vipengele vya
vya Best Collaboration Of the Year kupitia wimbo wake, African Beauty, pia
ameshinda kama Best Male Artist of the Year, huku Rayvanny akishinda kama
Best Vocalist of the Year.
Ukiachana
na hilo mwaka huu kwa mara ya kwanza Nandy ameweza kushiriki tamasha la One
African Music, Dubai. Amefanya show kadhaa nchini Marekani, pia anatarajiwa
kuonekana kwenye msimu mpya wa Coke Studio Afrika.
9.
Rostam
Kundi
hili la muziki wa hip hop linaloundwa na Roma na Stamina kwa mwaka jana
liliweza kutoa nyimbo mbili ambazo ni Hivi Ama Vile na Kiba_100 ambao
ulikuja kufungiwa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) kutokana na kukiuka
maadili, pia ulipelekea Roma kufungiwa kufanya muziki kwa kipindi cha miezi
sita adhabu iliyokuja kuondolewa kabla ya muda huo.
Walianza
mwaka kwa kuachia ngoma, Now You Know wakimshirikisha rapa kutoka nchini Kenya,
Khaligraph Jones ambaye ameshafanya kazi na wasanii kadhaa wa Tanzania kama
Rayvanny, Young Killer, Rosa Ree, Stereo na wengineo kibao.
Baada
ya hapo wakatoa wimbo mwingine uitwao Parapanda ambao ndio umefanya vizuri
zaidi kati ya nyimbo tatu walizotoa mwaka huu. Licha ya kutotoa video ya
wimbo huo, umeweza kufikisha views Milioni 1.5 katika mtandao wa YouTube tangu
ulipotoka August 02, 2018.
Rostam
ambao wanafahamika kwa kufanya show zenye ubunifu wa hali ya juu, mwaka huu
wameendeleza hilo kwenye majukwaa mbalimbali makubwa waliyopanda kutoa
burudani, pia ni kundi ambalo limefanya show nyingi zaidi kwa mwaka huu.
10.
Weusi
Si
mwaka huu pekee, kwa kipindi cha miaka kadhaa kundi la Weusi limekuwa likifanya
vizuri na hata linapokuja sula la kutoa wimbo kwa msanii moja moja (solo
project). Kundi hili ambalo linaundwa na wasanii watano, mara nyingi Joh
Makini, Nikki wa Pili na G Nako ndio wamekuwa wakisikika zaidi lakini kwa mwaka
huu wamebadili hilo.
Bonta
na Lord Eyes kwa mwaka huu wameweza kusikika kwenye nyimbo za kundi hilo. Bonta
amesikika kwenye wimbo uitwao Mdundiko, huku Lord Eyes akitamba kwenye ngoma,
Swagire.
Utakumbuka
tangu kuundwa kwa kundi hili ni wimbo mmoja tu ambao umeweza kuwakutanisha
wasanii wote, wimbo huo unakwenda kwa jina la Watoto wa Mungu.
Mwaka
jana walipanda jukwaa moja na rapa kutoka Marekani, Future alipokuja Tanzania.
Mwaka huu pia wameweza kushiriki kwenye show kubwa na kufanya vizuri na umekuwa
ni utamaduni wao kwa kipindi kirefu sasa.
Kutokana
na kufanya kwao vizuri, pia mwaka huu wameendelea kupata mikataba minono ya
kuwa mabalozi wa kampuni mbalimbali kwa lengo la kutangaza biashara za kampuni
hizo. Ni wasanii wachache sana wanaoweza kupata nafasi kama hizo tena kwa
kipindi kirefu kama ilivyo kwao.
Imeandikwa
na Peter Akaro