F Johari awakingia kifua warembo Bongo Movie tuhuma za kuchukua waume za watu | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Johari awakingia kifua warembo Bongo Movie tuhuma za kuchukua waume za watu


Msanii wa filamu Bongo, Johari amefunguka kuhusu kashfa za wasanii wa Bongo Movie kuiba wake na waume za watu kwa kusema suala hilo halipo kwenye tasnia ya uingizaji pekee.

Muigizaji huyo amesema wale wanaoeneza hilo hawajafanya utaviti wa kutosha kwani ni vitu ambavyo vipo sehemu mbali mbali kwenye jumuiya ya watu.

"Sehemu yoyote yenye mkusanyiko wa watu mbalimbali na rika tofauti haya mambo yanatokea kwa sababu kila mtu anatabia zake" amesema.

Ameendelea kuwa  sifa hizo wanasemwa wasanii wa Bongo Movie kwa sababu kwao yanaonekana zaidi, ila hata watu wengine wanafanya mambo makubwa tu.