F Zijue faida zitokanazo na kutumia chenza | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Zijue faida zitokanazo na kutumia chenza


Chenza ni tunda jamii ya chungwa. Licha ya kuwa maeneo mengi yanayostawishwa machungwa, machenza nayo hupatikana lakini si mengi kama machungwa.

Kama mara nyingi ninavyozungumza katika mada zangu mbalimbali kuwa ukimwuliza mtu kwanini una kula chenza atakuambia kwa kuwa ni tunda tamu lakini hawezi kukuambia faida zilizomo ndani ya tunda husika.

Ila siku ya leo nitakueleza japo kwa uchache faida zitokanazo na chenza kama ifutavyo;

1. Tunda hili ni tamu lina faida nyingi sana katika mwili wa binadamu ikiwemo kuongeza vitamin C,

2. Pia linazuia kuvuja damu katika fizi kwa watu wenye matatizo ya kutokwa na damu katika fizi za meno yao.

3. Vilevile tunda hili lina imarisha mifupa, linaongeza nguvu katika miusuri nakuondoa maumivu ya viungo.

4. Pia linaondoa baridi yabisi, linaondoa viuvimbe chini ya tumbo, linasaidia kuondoa mawe katika figo na kibofu, linatibu unene na mirija ya damu na kutibu udhaifu wa macho.

Mara nyingi watalamu wa afya wanashauri kula tunda lenyewe lililowiva tu kwa sababu hili ndilo limesheeni wingi wa faida lukuki kama ambavyo tumeeleza hapo juu.