Mzunguko wa pili wa Ligi kuu ya Vodacom kuanza leo ambapo timu ya simba itakutana kuonyeshana ubavu na JKT Tanzania mchezo utakao pigwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaamu saa 10:00 jioni.
Katika mzunguko wa kwanza simba wameshinda mechi 16, sare 2 na kupoteza mchezo 1, wakati JKT Tanzania mzunguko wa kwanza wameshinda michezo 7, sare 6 na kupoteza michezo 6.