F Halmashauri ya Rorya yapokea sanitizer kutoka Rorya forum ili kujikinga na corona | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Halmashauri ya Rorya yapokea sanitizer kutoka Rorya forum ili kujikinga na corona


Na Timothy Itembe Mara.

HALMASHAURI ya Rorya mkoani Mara jana katika Baraza la madiwani wamepokea vifaa vya Sanitizer kutoka kikundi cha Rorya Forum ikiwa ni kuunga juhudi za Serikali katika kupambana na ugonjwa hatari wa Corona.

Akipokea vifaa hivyo kwa ajili ya halmashauri Mwenyekiti,Albeth Machiwa alitumia nafasi hiyo kushukuru kikundi hicho ambapo alisema kuwa Chupa moja ina uwezo wa kuokoa uhai wa Mtu.

“Niwashukuru Ndugu zangu kwa msaada mliutoa ndani ya halmashauri yetu kwa hali hiyo milango ipo wazi kwa wadau wengine wa maendeleo kuja na kushirikiana nasi katika shuguli za maendeleo vifaa mlivyo toa vina mchango mkubwa katika halmashauri yetu ambapo Chupa moja ina uwezo wa kuokoa uhai wa Mtu katika kufanya  hivyo ni moja ya maendeleo kwa watu wa Rorya na Tanzania kwa ujumla “alisema Machiwa.

Mmoja wa kikundi hicho,George  Nyamasi kwa niaba ya wenzake alisema kuwa kindi hicho kimewiwa na maendeleo ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa wa Corona ambapo wametoa Sanitizer kwa watumishi wa Hospitali,Vituo vya Afya na Zahanati waliopo wilayani hapo ilikujikinga na COVID 19.

Nyamasi aliongeza kuwa vifaa walivyokabidhi Halmashauri ya Rorya vina dhamani ya zaidi ya shilingi milioni moja na kuwa watendelea kutoa misaada katika halmashauri hiyo kulingana  na jinsi watakavyokuwa wanabarikiwa na  Mwenyezi Mungu.

Mganga mkuu wa halmashauri hiyo,DR Peter Mkenda aliwapongeza kwa msaada waliotoa wanakikundi hao ambapo aliomba kuendelea kutoa misaada kulingana na jinsi watakavyokuwa wamewiwa ili kuokoa uhai wa watu.

Mkenda aliongeza kuwa Sanitizer walizopokea watagawa kwa watumishi wote bila kuwepo upendeleo na kuwataka wahudumu wa Afya kwendelea kujikinga na Corona huku wakitoa maelekezo ya kujikinga na ugonjwa huo kama yanavyotolewa na Wizara ya Afya.

Katika Baraza hilo Diwani kata ya Roche,Nixon Amolo  aliomba halmashauri yake kuitendea haki kata yake ya Roche kwa kuwakamilishia Wananchi wake miundombinu ya Maji pamoja na Zahanati ya Ng’ope ili wananchi wanufaike na matunda ya Nchi yao.

Naye Diwani kata ya Kitembe,Thomas Patrick Lissa aliomba halmashauri hiyo kuandaa mpango mathubuti kwa ajili ya makusanyo kutoka Chanzao cha Barrick ili kuongeza mapato.

Lissa alisema kuwa halmashauri ya Rorya wanayo haki ya kupata asilimia ya makusanyo ya mapato yah fedha kutoka Mgodi wa Barrick kutokana na kuwa Mgodi huo ipo Mara na pia wanachangia miundombinu ya Barabara katika kupitisha vifaa vyao kwenda Nyamongo huku maji ya sumu yanayotajwa kuadhiri Watu na mifugo  wanayatumia watu wa Rorya.

Katika swala hilo mkurugenzi wa halmashauri ya Rorya,Charles Chacha aliwataka madiwani kuwa wavumilivu  wakati hatua zingine zikichukuliwa kupitia mkuu wa mkoa Mara,Adamu Kigoma Malima.