F Rais wa Uturuki afanya mazungumzo na rais wa Urusi kwa njia ya simu | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Rais wa Uturuki afanya mazungumzo na rais wa Urusi kwa njia ya simu


Rais wa Uturuki Recep tayyıp ErdoÄŸan azungumza na rais wa Urusi Vladimir Putin kwa njia ya simu kuhusu masuala tofauti  katika ushirikiano uliopo kati ya mataifa hayo mawili.


Katika mazungumzo yao viongozi hao wamejadili kuhusu hatua ambazo zimekwishapigwa katika ushirikiano kati ya Uturuki na Urusi.


Uturuki na Urusi ni mataifa ambayo   yamepiga hatua kubwa katika  sekata tofauti ikiwemo katika sekta ya utalii.


Raia kutoka nchini Urusi ni miongoni mwa  watalii wengi ambao hutembelea Uturuki katika msimu wa kiangazi.


Uturuki na Urusi ni mataifa mabyo yanashirikiana katika sekta ya uchukuzi , nishati,  uchumi na vile vile katika  kupambana na maambukizi ya virusi vya corona.


Taarifa iliotolewa na kitengo kinachohusika na upashaji habari ikulu mjini Ankara  zimefahamisha kuwa  katika mazungumzo yao rais Putin na ErdoÄŸan wamezungumzia pia  hali inayoendelea nchini  Libya , ukanda wa Meidterania na mapambano dhidi ya virusi vya corona.


Rais Putin pia amezungumza kuhusu umuhimu wa mazungumzio kuhusu hali inayoendelea katika ukanda wa Mediterania  upande wa Mashariki.


Kwa kumalizi mazungumzo yao , rais ErdoÄŸan na rais Putin  wanejadili kuhusu Syria na kusema kuwa  harakati za kidiplomasia kupatia suluhisho hali inayoendelea nchini Syria kupatiwa suluhisho.


Post a Comment

0 Comments