F Wanasayansi waonya juu ya kutokea kwa ‘mkasa mwingine wa volkano’ DRC | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Wanasayansi waonya juu ya kutokea kwa ‘mkasa mwingine wa volkano’ DRC


Wanasayansi wanaonya kuwa hatari ya mlipuko wa volkano kama ule wa 2002 inaweza kutokea tenaImage caption: Wanasayansi wanaonya kuwa hatari ya mlipuko wa volkano kama ule wa 2002 inaweza kutokea tena

Wanasayansi wanaonya kuwa ziwa la lava linajaa kwa kiwango cha kutishajuu katika Mlima wa volcano wa Nyiragongo uliopo juu ya mji wa Goma Mashariki mwa Jamuhuri ya kidemokrasi ya Kongo.

Mwezi Januari 2002, lava iliyomwagika ilimwagika kutoka Mlima Nyiragongo kwa kasi hadi katika mji wa Goma na kusababisha vifo vya watu 250 na kuharibu 20% ya mji wa Goma.

Kikundi cha wanasayansi wanaochunguza matukio ya milima, wameonya kuwa “mwamba unaoyeyuka unaweza kulipuka tena kupitia kuta za ziwa la volkano”, imesema taarifa yajarida la kisayansi.

“ Sasa, hali inaonyesha dalili za mkasa mwingine” Dario Tedesco, mtaalamu wa volcano na milima aliliambia jarida la masuala ya kisayansi.

Mtoto akitembea kando ya lava iliyoyeyuka katika uwanja wa ndege wa Goma, mwaka 2002Image caption: Mtoto akitembea kando ya lava iliyoyeyuka katika uwanja wa ndege wa Goma, mwaka 2002

Tathmini yao inaonesha kuwa hatari kubwa zaidi yam lima huo itatokea katika kipindi cha miaka 4, ingawa wanaamini tetemeko la ardhi linaweza kusababisha mlipuko huo mapema

“Hii ni volkano hatari zaidi duniani!” Profesa Tedesco aliongeza. Watu wapatao milioni moja wanaishi katika mji wa Goma.

Post a Comment

0 Comments