F NATO kushauriana kuondoka Afghanistan ama la | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

NATO kushauriana kuondoka Afghanistan ama la


Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema katika Mkutano wa Mawaziri wa Ulinzi wa NATO utakaofanyika mnamo Februari 17-18, NATO itatathmini ikiwa itabaki au kujiondoa Afghanistan.

Stoltenberg alijibu maswali ya waandishi wa habari kabla ya mkutano wa siku mbili utakaofanyika kwa ajili ya video.

Akibainisha kuwa hangeweza kutabiri matokeo ya mkutano huo, Stoltenberg alisisitiza kuwa mashauriano yanaendelea kuhusu Afghanistan na kwamba washirika wote wanaunga mkono mchakato wa amani nchini humo.

Stoltenberg amezitaka pande zote nchini Afghanistan kuona mchakato wa amani kama fursa ya kihistoria na kufanya mazungumzo kwa nia njema.

"Nataka kutoa ujumbe ufuatao. Wataliban lazima wapunguze vurugu. Lazima wazingatie ahadi zao kwa kufanya mazungumzo kwa nia njema na kuachana na vikundi vya kigaidi vya kimataifa kama vile Al Qaeda." Stoltenberg alisema kuwa NATO itaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo chini humo.

Alikumbushwa kwamba wanajeshi wote wa kimataifa wanapaswa kuondoka kutoka Afghanistan mnamo Mei 1 kulingana na makubaliano ambayo Marekani ilifanya na Taliban, Stoltenberg alijibu swali la ikiwa suala hilo bado linawezekana na kusema:

"Lazima tulinganishe kati ya kukaa kwa muda mrefu na kuondoka mapema mno. Hatuwezi kuruhusu Afghanistan igeuke kuwa bandari ya mashirika ya kigaidi tena. Tutatathmini kila mara idadi ya wanajeshi. Tulipunguza uwepo wetu. Miaka michache iliyopita, Wanajeshi wetu elfu 130 walikuwa katika shughuli za kupambana. Na wako kwenye misheni ya mafunzo na ushauri. Tumeweza kuwa huko kwa idadi ndogo sana kwa ajili ya kuwasaidia Waafghan kujenga uwezo wao wenyewe. "

Staltenberg alikumbushia kuwa Taliban inahusika na vurugu nchini Afghanistan, na kuongez kwa kusema,

"Tutashauriana, tutachukua hatua kwa uratibu na kufanya maamuzi pamoja. Tulikwenda Afghanistan pamoja kama washirika, tutafanya mipango pamoja, na tutaondoka pamoja wakati ukifika." 

Post a Comment

0 Comments