F Waziri wa biashara wa Burundi afutwa kazi kotokana na mauzo ya ndege | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Waziri wa biashara wa Burundi afutwa kazi kotokana na mauzo ya ndege


Waziri wa biashara, uchukuzi , viwanda na utalii, Immaculée Ndabaneze amefutwa kazi " kwa kuuweka uchumi haarini na kuchafua picha ya nchi ".

Alikamatwa kwa muda, akahojiwa na kuachiliwa Jumapili huku uchunguzi ukiendelea kuhusu madai hayo.

Bi Ndabaneze anakabiliwa na shutuma za ufisadi kuhusu mauzo ya ndege ya shirika la ndege la Burundi, Air Burundi.

Ndege hiyo iliuzwa kati ya mwezi Disemba 2020 na Januari 2021 “kwa mfanayabiashara wa Afrika Kusini kwa bei ya chini”, limeandika Shirika lisilo la kiserikali (NGO) linalopambana na ufisadi nchini Burundi, Olucome-Burundi kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Bi Ndabaneze hajajibu lolote kuhusu tuhuma hizo dhidi yake.

Post a Comment

0 Comments