Baadhi ya wafuasi wa kundi la waasi nchini Niger walifanya maandamano nje ya bunge la huku wakiwa wamebeba bendera za Urusi.
Baadaye baadhi ya waandamanaji walishambulia makao makuu ya chama cha rais aliyepinduliwa Mohamed Bazum na kuyachoma moto.
Urusi imeyaita mapinduzi hayo nchini Niger kuwa ni hatua ya kupinga katiba.
Urusi, pamoja na nchi nyingine, zimetoa wito wa kuachiliwa huru kwa rais Bazum aliyeondolewa madarakani, ambaye anashikiliwa na wapiganaji hao.
Kwa sasa haijulikani ni nani anayesimamia nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
Kamanda wa jeshi alijitokeza kuunga mkono wapiganaji, kwa maneno yake, ili ‘’kulinda umoja wa majeshi’’
Serikali yenyewe haijatangaza nani anaongoza.
Tangazo la usiku wa manane la kuondolewa kwa rais huyo lilirudiwa kwenye televisheni ya taifa, likiingiliana na muziki wa kizalendo na mistari kutoka Koran.
Kipindi cha habari, ambacho kwa kawaida hupeperushwa wakati wa chakula cha mchana, hakikutangazwa wakati huo.
Hata hivyo, katika mji mkuu wa Niger, Niamey, maduka na masoko yalifunguliwa tena katika muda wa kawaida, na wafuasi wa kundi hilo waliingia mitaani asubuhi.
Mamia ya watu walikusanyika nje ya jengo la bunge. Baadhi walipeperusha bendera huku wengine wakibeba mabango yaliyoandikwa "Ufaransa chini!" na "Kambi za kigeni!".
0 Comments