F Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko wajivunia mafanikio kitaaluma | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko wajivunia mafanikio kitaaluma


Na Heri Shaaban 

Shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko wilayani Ilala, wajivunia mafanikio kitaaluma inafanya vizuri kila mwaka  katika matokeo yake ya sekta ya Elimu.

Akizungumza katika mahafali ya kumi na tano ya shule ya Sekondari Uhuru Mchanganyiko Mkuu wa shule hiyo Jamaldini Hassan Mohamed, alisema mwaka 2023 matokeo ya kidato cha nne ufaulu ulikuwa asilimia 78 na matokeo ya kidato cha pili ufaulu asilimia 98 hivyo wana imani kubwa wanafunzi wanahohitimu leo watafanya vizuri zaidi.

Mkuu Jamaldini Haassn  alisema shule hiyo ilianza rasmi mwaka 2007 ikiwa na wanafunzi 160 na walimu nane wanafunzi wa kwanza walihitimu mwaka 2010 wanafunzi wahaohitinu mwaka huu 2024 jumla 436 ambapo wanafunzi hawa 237 ni Wavulana na wasichana 199 .

"Shule yetu ya Uhuru Mchanganyiko ina mafanikio makubwa kitaaluma na mwaka huu tumejipanga kufaulisha wanafunzi wote  kutokana na maandalizi yao kuwa mazuri kwa ushirikiano wa Walimu wangu na wazazi "alisema Mwalimu Jamaldini.

Alitumia fursa hiyo kuwapongeza Benki ya NMB na Menejiment yake  kwa kuiwezesha shule hiyo  meza 100 na viti 100 ambapo msaada huo umesaidia sana mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji  

Alisema kupitia msaada huo wa thamani za kujifunzia wamezihirisha kwa vitendo kauli mbiu ya Benki ya NMB haimuachi mtu pia imeunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya sita ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi wa Uhuru Mchanganyiko kuwa mabalozi wazuri huko wanapoenda wakatangaze mazuri ya Shule hiyo na  kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi ya mitihani iliyombele  yao kujiepusha na makundi yasio faa .

Aliwataka wawe na maadili mema  wasiingie katika mmomonyoko wa maadili washirikiane pamoja na wazazi waweze kusonga mbele kielimu kwani Taifa ili liweze kuendelea lazima watu  wake waweze kusoma

 Meneja wa Benki ya NMB KARIAKOO  Wiliam Nkuna alisema changamoto za shule hiyo watazitatua hivi karibu  NMB ina shughulikia shughuli za kijamii ikiwemo sekta ya Elimu.

Post a Comment

0 Comments