F Mafanikio ya ziara Rais Samia mkoa wa Tanga | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Mafanikio ya ziara Rais Samia mkoa wa Tanga

 


NA REBECA DUWE TANGA

MKUU wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Buriani ameeleza miradi mikubwa ikiwemo Bandari uliogharimu Bilion 429 Ambayo ilitembelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samaia Suluhu Hassan  alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi mikoani  Tanga .

Akizungumza  na waandishi w habari ofisini kwake alisema kuwa ujio Rais Dkt Samia  umeweza kufumbua mazuri mengi kwa wakazi wa mkoa wa Tanga kwani wengi walikuwa wanatamani wangesikia samaiaazungumze na wananchi  na kusikia kutoka kwa mama Samia.

Aidha kwa Mujibu wa Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema kuwa mnamo tarehe 22 feburary mwaka huu ndio Mh.Rais Dkt Samia  kuanza ziara Yake  kuazindua Hjospitali ya wilaya Handeni ambapo wananchi wengi waliojitokeza  na kumsikiliza Dk mama Samia kwa kazi kubwa iliyofanya a serikali yake.

Alisema kuwa watu wengi waliojitokeza wakiwemo wafanya biashara, bodaboda, viongozi wa dini,wasanii  Kinamama wa Tanga ambapo walimpokea kwa baibui la ukaya na hivyo hivyo imani ya wanatanga imekuwa kubwa kwake kwa ushirikiano waliouonyesha.

Mkuu wa mkoa Tanga alieleza miradi  Michache ambayo Mama samia alitembelea na kuzindua ndani  wilaya za mkoa wa Tanga,ambayo imegharimu  trillion 1 na milioni Mia nane  , ikiwemo mradi wa jengo la utawala Bumbuli wilaya Lushoto  jengo la  utawala Handeni Mji.

 Sambamba na hayo Balozi Buriani alisema Dkt. Samai alizindua mradi wa  Kilimo cha  Umwagiliaji katika wilaya ya Korogwe ambao uligharimu sh. bilioni 18. lego kuu ni wakazi wa Korogwe ambao ni wakulima mpungu kunufaika na kuongeza tija.

"Mradi shule ya Sayansi ya umahiri  ya wasichana katika Wilaya ya Kilindi mkoani humo ambapo serikali  ya awamu ya Sita imedhamiria kuboresha elimu kwa wasichana lakini pia itainua wilaya yetu kilindi kwani hata huduma muhimu serikali  ishaanza kupeleka maji ikiwemo huduma ya Maji ambapo wakala wa maji vijijini Ruwasa wamepeleka maji lakini pia kuna mpango uliowekwa tayari wankuleta maji Mvomero .,"

Mradi mwingine ni Barabara ya Tanga Pangani Saadani bagamoyo ambao inaruti tatu ambapo  ruti ya  kwanza bilioni 98 ruti ya  ya pili biioni 92 ruti Tatu bilioni 94 hivyo inaweza kusaidia kwenda kuondoa changamoto ya usafiri kwa watanzania  kwani hata wananchi wa pangani walikuwa wanatumia  Pantoni lakini daraja linaanza kukamilika. " Ameeleza mkuu wa mkoa Tanga Blozi Buriani.

Ambao miradi ya maji  serikali ya Samia  imeleta mradi miji 28 ambao unasimamiwa naTanga uwasa , lakini pia mkinga kuna mradi maji ambao maji yake yanatoka mto  zigi,katika wilaya Handeni maji ya msitu wa Bondo ambao unapeleka maji kwenye mto zigi  .
Aidha kutokana mradi huo maji pia miongoni wanufaika ni wanafunzi wa shule ya sayansi ya wasichana wilaya ya kilindi ambao tayari wamepata maji  safi na salama.

sambamba na hilo Rais Samia aligawa   mtingu ya gesi elfu 21 ,ambapo ni ugawagiji wa majiko ya ruzuku ambayo imeuzwa kwa sh.17000, hivyo serikali imezingatia  kujali mazingira na mabadiliko ya Tabia ya nchi lengo kuu ikiwa ni kuhamasisha nishati safi.

Mkuu wa mkoa w Tanga  alielezea kuwa Kampuni ya mafuta ya GBP  ambayo inazalisha Lita milioni 200 ambayo ilikuwa imekusudiwa kusaidia mikoa ya kaskazini yatumia Tanga iii kuweza kutekeleza agizo la serikali lakini Sasa Kampuni hiyo imefanya uwekezaji wa gasi ambayo itauw na uzalizaji mkubwa wa  mara mbili zaidi makumpuni yote yanayotengeneza gasi.




 

Post a Comment

0 Comments