F Mwenyekiti Mpete ajumuika na Waislamu katika Sala ya Eid,ahimiza Watanzania kudumisha amani | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Mwenyekiti Mpete ajumuika na Waislamu katika Sala ya Eid,ahimiza Watanzania kudumisha amani









Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe ambaye ni diwani wa kata ya Utalingolo Erasto Mpete amejumuika pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislam kwenye Sala ya Eid Al Fitr katika Msikiti wa Madina uliopo Idundilanga mjini Njombe leo March 3,2025.

Mpete ametumia abada hiyo kutoa wito kwa watanzania kuendelea kudumisha amani.

"Nimekuja hapa kwasababu wote ni watanzania na tudumishe amani na kudumisha amani ni kama hivi tulivyokutana katika ibada na kushirikiana"amesema Mpete

Kwa upande wake Shekhe wa Mkoa wa Njombe Rajab Msigwa ametoa wito kuyaenzi mafundisho  yaliyotolewa wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani hata baada ya kumaliza funga. 

"Tumekuwa wenye nidhamu sana katika mwezi mtukufu wa Ramadhani nidhamu hii  ndio mafundisho ambayo Mwenyezi Mungu anatuhitaji tuishi nayo katika miezi kumi na moja inayokuja kwa hiyo sote tukizingatia mafunzo haya tutaendelea kuishi vizuri"amesema Msigwa

Siku kuu za Eid el Fitir husherekewa baada ya kutamatika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani katika kipindi cha mwezi mmoja mara baada ya mwezi kuandama.

Post a Comment

0 Comments