F RUWASA watekeleza azma ya serikali kumtua mama ndoo kichwani | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

RUWASA watekeleza azma ya serikali kumtua mama ndoo kichwani


Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani ameeleza kuwa zaidi ya shilingi Trillion 1.2 zimeenda kwenda sekta ya maji katika mkoa wa Tanga ambayo ni fedha iliyotolewa na Rais Dkt Samia  Suluhu Hassan kwa kuondoa changamoto ya ukosefu wa maji  kwa wananchi wa mkoa Tanga.

Balozi Dkt.Batilda aliyasema  hayo wakati akizindua program ya kitaifa ya visima 900 inayolenga kuhakikisha zaidi ya asilimia 85 ya wananchi wa maeneo ya vijijini kupata huduma ya maji safi na salama na kutimiza azma ya serikali ya kumtua mama ndoo kichwani.

Aidha Balozi Dkt. Batilda alizindua mradi huo katika kijiji cha Makorora kata ya Magoma wilaya Korogwe ikiwa na lengo mradi huo ni kutekeleza azma serikali ya kuondoa changamoto ya majikwa wananchi ambapo mapa Sasa wilaya ya Korogwe inanufaika na mradi huo katika vijiji vya Mwakinyumbi Station Makorora kwaisewa,Makoya ,Buiko,Ngombezi na kilole kwa mzee.

Akisoma taarifa ya mradi Meneja wa wakala wa maji vijijini Ruwasa Wilaya  Korogwe Injinia  Muharami Mohamed alisema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milion 656,472,450 kupitia fedha za Lipa kwa matokeo (pay for R na national fund.).


Mradi wa uchimbaji wa visima  umekamalika kwa alisimia 100 ambapo  ujenzi wa visima  umekamilimika kwa asilimia  85 kwa ajili ya kutekeleza  azma ya serikali ya kuondoa changamoto ya ukosefu wa maji vijijini vya Mwakinyumbi Station, Makorora Kwaisewa, Makoya, Buiko Ngombezi,Kilole kwa mzee na Mgambo.

Lengo la serikali katika wilaya ni kufikia wanannchi wapatao 9450 ambapo kwa Sasa upatikanaji  wa maji umeongezekq hadi kufikia asiliamia 69.9 alikini ujenzi huo wa visima vya maji umeweza kunufaisha wananchi  wapatao 50 kupata ajira ya mud mfupi

Kwa upande wake Meneja wa wakala wa maji vijijini Ruwasa  Injinia Upendo  Lugongo  aliwaadi wananchi wananchi wote kufikiwa na huduma za majivkupitia mtandao huo ndani ya muda mfupi kwamba watu wote watakunywa na kuoga maji safi na salama


 

Post a Comment

0 Comments