F WADAU WA USAFIRISHAJI MAJANI KUTOFUATA SHERIA NA TARATIBU ZILIZOPO NI CHANGAMOTO | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

WADAU WA USAFIRISHAJI MAJANI KUTOFUATA SHERIA NA TARATIBU ZILIZOPO NI CHANGAMOTO


SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania Tasac, ambayo inayohusika na  udhibiti wa huduma za usafiri majini imesema kuwa miongoni mwa changamoto  kubwa   iliyopo ni wadau wanaowahudumia kutokufuata utaratibu na sheria  hususani wanapoomba leseni.

Hayo aliyasema  mkurugenzi wa udhibiti wa usafiri kwa njia ya maji wa shirika la uwakala wa meli Tanzania  TASAC  Nelson Mlali wakati wa mafunzo ya elimu  kwa watoa  huduma ambao ni  wale wanaowadhibiti ili wa wawe na uelewa mkubwa juu ya huduma  hizo wanazotoa.

Alisema lengo kuu la kutoa elimu hiyo ni kuleta uelewa kwa wahusika ambao ni Mamlaka  ya  Bandari  Tanzania  TPA, Wakala wa forodha na meli,wanaokusanya mizigo na kupunguza migogoro  inayotokea baina ya watoa huduma.

  "Wapo watu wasiowaamimifu ambao wanashindwa kufuata utaratibu na sheria hivyo kupitia elimu hii tunawapa uelewa wa madhara ambayo yatatokea wasipofuata utaratibu na kuweza kupata  kupunguza changamoto hizo".alisema Mlali

Sambamba na hayo Mlali alitoa wito kwa watoa huduma kushirikina katika Majukumu kwa sababu wote katika jukuma la kufikisha huduma ili kuweza kupunguza malalamiko na migororo inayotokana na ukiukwaji wa sheria.

"Majukumu wa TASAC katika udhibiti wa huduma za usafiri  wa majini ni kutoa ,kuhuisha na kufuta leseni za watoa huduma katika sekta ya bandani na usafiri kwa njia maji. lakini pia tumeweka kanuni na masharti ya kufuatwa na watoa huduma  wanaodhibitiwa ."aliongeza  MLali.

Mlali alisema kwa kutofuata Sheria na taratibu za utoaji wa huduma kwa wadau hao kutashusha kiwango cha ufanisi AA bandari zilizopo hapa nchini na kuifanya kuingia kwenye ushindani na nchi nyingine hali ambayo inaweza kupelekea wafanyabiashara kwenda kufanya kazi nje.

"Lengo letu kubwa ni kukaa nao tuone ni maeneo gani ambayo hayafanyi vizuri  ili waweze kufanya vizuri kwaajili ya faida ya bandari zetu hapa nchini tungependa pia tupunguze malalamiko, migogoro na ucheleweshwaji wa utoaji huduma za usafiri kwa

Kwa upande wake Afisa mfawidhii kutoka shirika la uwakala wa' Meli Tanzania 'TASAC' mkoa wa Tanga Christopher Shalua  amewataka wadau wa usafirishaji kwa njia ya maji kuhakikisha kupitia sekta zao za afya wanazingatia usalama kabla na baada ya kutoa huduma za kupakuwa na kupakia mizigo kweli Meli hususani zinazotoka nje ya nchi.

"Eneo la bandari ni eneo ambalo Lina mashara mengi kuna taasisi ambazo zinafanya kazi zao bila kujua kwamba wanaweza wakaingiza magonjwa hapa nchini Kuna baadhi ya takataka zianzokuja kwetu kwa njia ya Meli zinazotoka nje watu wa sekta ya afya lazima wahakikishe kwa nafasi zao  hakuna madhara yanayotokea kwenye nchi yetu kupitia vyombo tunavyohudumia" alisisitiza Shalua.

Aidha afisa huyo amewataka wadau wote wa usafirishaji kwa jia ya maji kuhakikisha  wanafuata Sheria na taratibu za nchi ikiwemo kuhusiaha lwseni zao ili waweze kupata ruhusa ya kufanya kazi zao  bandarini wakati wote.

"Mawakala na wadau wote  wanaotoa huduma za bandari lazima kuhakikisha kuwa vibali vyao vinahuishwa  ili kufuata taratibu na Sheria za nchi yetu  katika utoaji wa huduma bandarini" ameongeza

Post a Comment

0 Comments