RPC Katabazi akabidhi vitimwendo 20 vilivyotolewa na BAKWATA.


Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Manyara SACP George Katabazi amekabidhi viti mwendo 20 kwa watu wenye uhitaji maalumu vilivyotolewa na Baraza la  waislamu mkoa wa Manyara BAKWATA.

Kamanda Katabazi amewaomba watumiaji wa hizo viti mwendo wazingatie Sheria za Barabarani kwasababu baiskeli hizo zitakuwa zinatumika Barabarani ambapo kutakuwa na watumiaji wengine wa Barabara ili waweze kuepuka ajali za Barabarani.

Pia ameendelea kusemakuwa jeshi la polisi lipotayari kuwalinda kwasababu jukumu la jeshi la polisi ni kulinda raia na Mali zao lakini ulinzi huo siyo wa jeshi la polisi pekee hata viongozi wa dini wadau mbalimbali Taasisi pia wanajukumu la kuwalinda watu hao wenye uhitaji

Naye shekhe wa mkoa wa Manyara Mohamed Kadidi amewahasa walezi wa watu hao kuwa watunzaji wa viti hivyo ili kuweza kudumu navyo kwa muda mrefu huku akiendelea kusema kuwa Taasisi na wadau mbalimbali waendelee kujitokeza kusaidia wenye uhitaji

Post a Comment

0 Comments